top of page
To see this working, head to your live site.
UUYK FORUM
Chagua Forum Hapa Chini Na Kisha Ungana Na Wapendwa Wenzako Katika Hoja Mbalimbali.
Hapa ni Kwa Ajili Ya Nyimbo,Mijadala,Maswali Na Hoja Zote Zinazohusu Mziki Wa Injili
Hapa Ni Kwa Ajili Ya Watu Wote Wenye Shida Mbalimbali Na Wanahitaji Ushauri Wa Kiroho Na Kimwili Pia
Sehemu hii ni kwa ajili ya maombi kwa wenye shida mbalimbali, Pamoja na Wale Wanao Hitaji Maombi
Hapa Ni Kwa Ajili Ya Watumishi Wote Pia Unaweza Kukutana Na Watumishi Hapa Kwa Urahisi Zaidi
New Posts
- Noel Isaya MwakibeteAug 22NENO LA LEOHebu tuweze kuangalia vile Bibilia inaelezea upendo, na kisha baadaye tutaangalia namna chache vile Mungu ni sehemu kuu ya upendo. “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabiri; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wo wote” (1Wakorintho 13:4-8a).Hii ndilo elezo la juu sana la Mungu kuhusu upendo, na kwa sababu Mungu ni upendo (1Yohana 4:8) hivi ndivyo ilivyo. Upendo (Mungu) hajilazimishi/haujilazimishi kwa mtu yeyote. Wale wanaokuja kwake wanafanya hivyo kwa kuitikia upendo wake. Upendo (Mungu) huonyesha upole kwa watu wote. Upendo (Yesu) alizunguka kote akifanya mazuri kwa watu wote bila upendeleo. Upendo (Yesu) hakutamani kitu cha wengine walikuwa nacho, aliishi maisha ya unyenyekevu bila kunung’unika. Upendo (Yesu) hakujivunia vile alivyo kuwa kimimwili, ingawa aliweza kumshinda nguvu kila mtu aliyekutana naye. Upendo (Mungu) haulazimishi unyenyekevu. Mungu hakulazimisha Mwnawe kunyenyekea, lakini kwa mubadala Yesu kwa pendo lake alimtii Babaye wa mbunguni. “Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu” (Yohana Mtakatifu 14:31). Upendo (Yesu) alitwaza/na huwaza yaliyo mazuri kwa matakwa ya wengine. Tibitisho kuu la upendo wa Mungu limeelezwa kwetu sisi katika Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Warumi 5:8 yakiri ujumbe sawa na wa Yohana: “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.” Tunaweza kuona kutoka aya hizi kuwa nia kuu ya Mungu ni tuwe pamoja naye katika mji wake wa milele, mbinguni. Ameifanya njia rahisi kwa kulipa gharama ya dhambi zetu. Anatupenda kwa sababu alichagua kwa kutekeleza kifungu cha nia yake. Upendo husemehe. “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” (1Yohana 1:9). Je inamaanisha nini Mungu ni upendo? Upendo ni sehemu kuu ya Mungu. Upendo ni sehemu kuu ya tabia ya Mungu, na utu wake. Upendo wa Mungu kwa vyovyote vile haugongani/hitilafiana na utukufu wake, utakatifu na haki yake hata gadhabu yake. Sehemu zote za Mungu kwa pamoja zimekamilika. Chochote Mungu anatenda hupendeza, haki kwa sababu kila afanyacho hukifanya kwa haki na usawa. Mungu ni mfano mtakatifu wa upendo wa kweli. Cha kushangaza, Mungu amewapa uwezo wa kupenda vile anavyo penda, kupitia nguvu za Roho Mtakatifu wale wote watakaomkubali Mwanawe kama mwokozi wa maisha yao. (Yohana 1:12; 1Yohana 3:1, 23-24).Like
- Michael Isaya MwakibeteJul 18MUZIKI WA INJILIkwa waimbaji wote unaweza kuonana nami nikakufanyia kazi nzuri kabisa karibuni wapendwa woteLike
bottom of page